Mlimani City Mall yatangaza zawadi ya X-Mas na Mwaka Mpya
Meneja Mkuu
wa Mlimani City, Pastory Mroso,((katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi
maalum wa promosheni ya “Fanya shomping Mlimani City ushinde Gari” katika
kipindi cha msimu wa sikukuu ya Chrismass na Mwaka Mpya.Kulia ni mwakilishi
kutoka Gaming board, Abdalah Singano.Wengine ni wafanyakazi wa Mlimani City.
Katika kusherehekea Sikukuu za X-Mas na Mwaka Mpya,
uongozi wa Mlimani City kwa kushirikiana na wafanyabiashara wenhye maduka
ndfani yake umetangaza ofa maalumu kwa wateja
wake wanataofanya manunuzi katika msimu huu wa sikukuu.
Ofa hiyo inatoa fursa ya kujishindia zawadi mbalimbali
ikiwamo gari jipya kabisa la kisasa aina ya Renault Kwid, lenye thamani ya Dola
za Marekani 8,500.
Zawadi nyingine ni Vocha za Manunuzi kwa washindi 10, zenye
thamani ya 100,000/- kila mmoja, ambao watapatikana kwenye droo zitakazokuwa
zikifanyika kila wiki.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam
jana, Meneja mkuu wa Mlimani City Ndugu Pastory Mrosso wa kila alisema kuwa washindi
wa kila wiki watafanya manunuzi katika duka lolote ndani ya Mlimani City kwa
kutumia vocha zao.
Promosheni hii maalumu imeanza Desemba 15 na inatarajia
kufikia mwisho Januari 7, 2017, ambapo droo ya kubwa ya kupata mshindi wa gari
itafanyika wiki ya pili ya Januari 2017.
Meneja huyo aliwaomba watanzania kuendelea kufanya
manunuzi yao katika maduka ya Mlimani City, kutokana na kuwajali wateja wake na
kutoa huduma zinazokwenda na wakati na hasa katika kipindi hiki cha X-Mas na
Mwaka Mpya
Post a Comment