Halotel yasherehekea mwaka mmoja kwa kuzindua huduma mpya
Kwa
kipindi hicho cha mwaka mmoja, Halotel imeweza kufikia malengo yake kwa kiasi
kikubwa ikiwamo kuongeza idadi ya watumiaji wa mtandao wake.
Kwa
mujibu wa Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), hadi kufikia Septemba mwaka huu,
ilikuwa na watumiaji wa mtandao huo wapatao milioni tatu na nusu.
Lakini
pia, ripoti ya robo ya kwanza na ya pili ya mwaka huu ya TCRA inaonesha kuwa, Halotel
imekua kwa kasi kwa upande wa ongezeko la wateja.
Akizungumza
na waandishi wa habari Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halotel
Tanzania, Lee Van
Dai, alisema, mafanikio ya kampuni hiyo yametokana na ushirikiano uliopo kati
ya wafanyakazi pamoja na ubunifu binafsi wa kibiashara wa kampuni hiyo.
Alisema
kuwa, kwa sasa Halotel ndio kampuni
pekee inayotoa huduma bora za mawasiliano (IT) kwa kampuni kubwa zikiwamo CRDB, NMB, BOA, FINCA, EXIM,
SNV-Southern Netherlands na Development Organization.
Kwa
mujibu wa Lee, Halotel ina vifurushi mbalimbali kwa wateja
wake kama vile Halo, Virushi vya wanafunzi, huduma maalumu kwa waajiri ya
makundi mbalimbali kama vile waajiriwa serikalini, wanajeshi, askari polisi na
walimu ambapo wanapata dakika 15 za mawasiliano bure kila siku.
“Lengo
letu ni kuhakikisha kwamba tunawapiku washindani wetu katika soko na ndio maana
huduma zetu zimekuwa zikipokewa vizuri sokoni. Tunajivunia kuwa kati ya kampuni
bora katika utoaji wa huduma za mawasiliano nchini.
“Kutokana na hali hiyo, tunaelekeza nguvu zetu zote katika kuboresha
miundombinu yetu. Kwa mfano, hadi sasa tumekwisha jenga zaidi ya kilometa
20,000 za mkongo wa mawasiliano na zaidi ya vituo 2,700 kwaajili ya kupokea
mawasiliano. Tumepeleka mitambo maalumu ya kuboresha mawasiliano katika vijiji
3,000 ambavyo awali havikuwa vimeunganishwa.
“Hiyo ni hatua ya kwanza ya kuhakikisha mawasiliano
yanaenea nchini Tanzania,” alisema.
Alifafanua zaidi kuwa lengo la Halotel ni kuongeza
idadi ya watumiaji kufikia milioni saba, ifikapo mwishoni mwa mwaka 2017, na
milioni tatu kwa watumiaji wa Halopesa.
Katika
hatua nyingine, Naibu Mkurugenzi Mkuu huyo, alitumia fursa hiyo kuzindua huduma
mpya ya Halopesa, huku akiwataka watanzania kujiunga na huduma hiyo, akidai
kuwa imeenea sehemu kubwa nchini na ni ya haraka.
Ili
kutumia huduma hiyo, mtumiaji anatakiwa kupiga namba *150*88#,
kisha kufuata maelekezo.
“Kwa
kutumia Halopesa mteja anaweza kufanya malipo mbalimbali kama vile kutuma na
kupokea fedha, kupokea au kutuma fedha kupitia benki na kulipia huduma nyingine
kama Luku, Dawasco, and TV subscription-ZUKU, GEPF, TCU na Polisi,” alisema.
Halotel imekuwa mstari wa
mbele katika kusaidia shughuli mbalimbali za kijamii. Hadai sasa kampuni
imefanikiwa kutoa ajira za moja kwa moja zipatazo 25, 000 na 1,300 za moja kwa
moja kwa watanzania.
Aidha kampuni inaboresha
miundombinu ya kijamii kama vile utoaji wa huduma ya bure ya mtandao wa
intaneti kwa shule 450, zenye umeme kwa miaka mitatu ijayo.
Kumekuwapo pia na ujenzi wa
vyumba vya kopyuta kwa ajili ya huduma ya intaneti kwa kutumia modem katika
Mikoa ya Pwani na Katavi.
Hivi karibuni Halotel imetoa
shilingi miliioni 15 kwaajili ya kusaidia wananchi wa Kagera waliokubwa na
tetemeko la ardhi.
Post a Comment