USIKU WA BI KIDUDE WAJA
bi kidude kuenziwa ziff,
usiku wa bikidude,
usiku wa wanawake ziff,
jukwaa la wanawake
Na Andrew Chale, Zanzibar
WANAMUZIKI
Nguli nchini wakiongozwa na Sit bin Saad ambaye ni mjukuu wa marehemu
Bi.Kidude,Synerg,Baby J wote hawa ni kutoka Zanzibar Linah na THT Band
kutoka Dar es Salaam kesho watawasha moto ndani ya mabo klabu kwa ajili
ya kumuenzi marehemu Bi.Kidude ambaye aliwahi kutumbuiza katika
matamasha ya ZIFF yaliyowahi kufanyika.
Tamasha
la filamu la nchi za Jahazi maarufu kama ZIFF linaendelea kupamba moto
na kesho ni usiku maalumu wa wanawake katika kumuenzi marehemu
Bi.Kidude katika tamasha hilo.
Tamasha
hilo ambalo lina siku ya 5 tangu kuanza kwake limekuwa ni kivutio
kikubwa kwa wakazi na wageni kutoka kila kona ya dunia kuwapa burudani
kulingana na mahitaji.
Usiku
wa wanawake unatarajia kufanyika jioni ya leo ndani ya Mambo klabu
ampapo wasanii watakao tumbuiza katika tamasha hio watakuwa ni wanawake
pekee ambapo mjukuu wa marehemu Bi.KIdude atafungua dimba kutoa
burudani hiyo.
Wanawake wameombwa kuhudhuria kwa wingi kwakuwa tamasha la siku ya leo ni kwa ajili ya wanawake.
katika
tamasha hilo la usiku wa wanawake wasanii hao wataweza kukonga nyoyo za
mashabiki wake na kufanya kufana kwa tamasha hilo ambalo linamkumbuka
Bi.kidude kwa mchango wake ambao alikuwa akiutoa katika kipindi chake
chote cha uhai wake.
Hata
hivyo burudani hiyo itaambatana na kuonyeshwa kwa filamu mbili tofauti
ikiwemo ya The Last Fishing Boat kutoka Malawi na Lilet never Happened
kutoka Netherland.
TBL YASAIDIA MIRADI YA MAJI YA SH. MIL 50 CHUO KIKUU CHA ST AUGUSTINE, SH. MIL. 49 MISUNGWI, MWANZA
Meneja
Mauzo wa Na Usambazaji wa TBL Kanda ya Ziwa, Malaki Staki wa kwanza
(kulia), kushoto kwake ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu
Agostino, Dkt,Charles Kitima, kwa pamoja wakitaka utepe kuzindua moja ya
matanki ya kuhifadhi maji,katika chuohicho.Mradi huo umetekelezwa na
TBL kwa gharama y ash. Milioni 50.
Makamu
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino (SAUT) Dkt Charles Kitima
kushoto akimshukuru Meneja Mauzo na Usambazaji wa TBL Kanda ya Ziwa,
Malaki Staki, muda mfupi baada ya kuzindua mradi wa matanki ya kihifadhi
maji chuoni hapo jana.Mradi huo wa ujenzi wa mantaki hayo mawili yenye
ujazo wa lita 100,000 kila kila mmoja umegharimu sh. Milioni 50.
Makamu
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine, Dkt Charles Kitima wa nne
kutoka kushoto, Meneja Mauzo na Usambazaji wa TBL Kanda ya Ziwa, Malaki
Staki, wa nne kutoka kulia wakiwa katika picha ya pamoja baada ya
kukabidhi matanki mawili ya maji kwa chuo hicho.Wa pili kutoka kulia ni
Askafu wa Jimbo Kuu Katoliki Mwanza, Askofu Yuda Thadeus Ruwa’ich.wa
kwanza , kulia ni Askofu Paul Luzoka .kulia kwa Dkt Kitima ni Padri
Mwanjonde.
Mkurugenzi
wa Uhusiano na Sheria wa TBL, Stephen Kilindo,akizungumza na baadhi ya
wenyeviti (hapo pichani) wa Vijiji vya Wilaya ya Misungwi ()muda
mfupi kabla ya kukabidhi hundi ya sh.49 milioni kwa ajili ya kukarabati
visima vya maji wilayani humo.Kushoto ni Mkurugenzi wa Halmshauri ya
Wilaya hiyo, Nathan Mshana na Meneja Mauzo na Usambazaji TBL Kanda ya
Ziwa, Malaki Staki.
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Misungwi, Nathan Mshana akizungumza na baadhi ya
wenyeviti wa vijiji wilayani humo (hawapo pichani), muda mfupi kabla
ya kukabidhiwa hundi ya shilingi milioni 49 kutoka Kampuni ya Bia
Tanzania (TBL)
Meneja
Mauzo na Usambazaji wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Kanda ya
Ziwa.Malaki Staki akimkabidhi mfano wa hundi Mkurugenzi wa Ufundi wa
kampuni ya Nyagama Investment Ltd Simon Mazuka, kwa ajili ya kutekeleza
mradi wa ukarabati wa visima 20 vya maji katika baadhi ya vijiji vya
wilaya ya Misungwi.Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria
wa TBL, Stephen Kilindo,wa pili ni kutoka kushoto ni Mhandisi wa Maji
Wilayani Misungwi,Jumanne Kitiku.Nyuma ya Malaki ni DED wa Halmashauri
ya Misungwi, Nathan Mshana na wa kwanza kushoto ni Afisa Mipango wa
Halmashauri hiyo,Pastory Mkaruka.
Meneja
Mauzo na Usambazaji wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Kanda ya Ziwa
Malaki Staki ,akiwa katika picha ya pamoja na wenyeviti wa baadhi ya
vijiji vya wilaya ya Misungwi ambao mradi ya ukarabati wa visima
utakaoanza kutekelezwa mapema mwezi huu, baada ya Kampuni ya TBL
kukabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 49.
Post a Comment