ad

ad

VODACOM YAZINDUA MASHINDANO YA MBIO ZA BAISKELI JIJINI DAR.

(katikati),Meneja udhamini na matukio wa kampuni ya Vodacom,Rukia Mtingwa (kushoto) na Mwenyekiti wa maandalizi wa mashindano hayo ya mbio za baiskeliyanayojulikana kama Vodacom Cycle Challenge,Nazir Manji wakizindu rasmi mashindano hayo yanayotarajiwa kufanyika jijini Mwanza hivi karibuni.Hafl ya uzinduzi ilifanyika kwenye ukumbi wa Idara ya habari MAELEZO Dar es Salaam

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi Nazir Manji (kulia) akizungumza na waandishi wa habari.

Mkuu wa udhamini wa Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom,George Rwehumbiza (wa pili kutoka kushoto) akizungumza na wandishi wa habari wakati wa uzinduzi huo.

Na Kambi Mbwana
MASHINDANO ya baiskeli yanatarajiwa kufanyika mjini Mwanza, Novemba 12 hadi 13 na kudhaminiwa na Kampuni ya Simu za Mikononi ya Vodacom, huku yakigharimu shilingi Milioni 50.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Udhamini wa Vodacom Tanzania, George Rwehumbiza, alisema kwamba mashindano hayo yameboreshwa kwa kiasi kikubwa.

Alisema kwamba waendesha baiskeli wajitokeze kwa wingi katika patashika hizo huku akisema yatakuwa na tija na faida kwa mchezo huo.

“Mashindano hayo yatafanyika kwa siku mbili Novemba 12 na 13, huku yakiwa ni mbio za kilomita 196 kwa wanaume, kilomita 80 kwa wanawake, huku walemavu wanaume wakishiriki mbio za kilomita 15 na wasichana kilomita 10.

“Shindano hili la Vodacom Mwanza Cycle Challenge ni mahususi kwa kukuza mchezo huu hapa nchini kwa lengo la kupata wawakilishi bora katika mashindano mbalimbali ya kimataifa,” alisema.

Mashindano hayo yanaandaliwa kwa mwaka wa tano na Vodacom Tanzania, huku yakidhaminiwa na Alphatel, TBL, Knigth Support na SBC, kupitia kinywaji chake cha Pepsi.

No comments