MAANDAMANO YA KUPINGA UJANGILI WA TEMBO NCHINI
Matembezi hayo ya kupinga ujangili yameandaliwa Bw. Patric Patel, Mkurugenzi, African Wildlife Trust (wanne kutoka kulia msitari wa mbele)
yakiwa na lengo la kuelimisha wananchi na Ulimwengu mzima kwa ujumla
juu ya madhara ya ujangili. Matembezi yamehusisha raia wa nchi
mbalimbali duniani.
Mhe. Lazaro Nyalandu (Mb) ambaye ndiye mgeni rasmi katika kilele cha matembezi hayo ametoa wito
kwa wananchi wote waendelee kushirikiana na serikali kupiga vita
ujangili kwa kuwafichua majangili popote wanapowaona; na taasisi zote za
umma zishirikiane kupambana na ujangili ili kuutokomeza kabisa.
Post a Comment